Kaimu
Meneja wa Abood Media Abeid Dogoli ameithibitishia zamastreet.com kwamba ni
kweli mtangazaji wa siku nyingi Tanzania
Julius Nyaisanga amefariki dunia leo asubuhi.
Amesema
Nyaisanga alipelekwa hospitali ya Mazimbu Morogoro jana saa nane mchana
kutokana na kusumbuliwa na Kisukari pamoja na presha ambapo asubuhi ya leo
October 20 2013 ndio akafariki dunia akiwa na umri wa miaka 53
Mara
yake ya mwisho kuingia ofisini ilikua juzi japo alikua ameanza likizo toka
October 12 ambapo huu ulikua ni mwaka wake wa tatu toka ameanza kufanya kazi na
Abood Media ya Morogoro kama Meneja wa kituo.
Taarifa
nyingine kuhusu msiba wake utaendelea kuzipata hapa millardayo.com
R.I.P
Uncle J
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni