Jumapili, Oktoba 20

ZAMASTREET: Kanye West azidi kuwaduwaza fans wake,na inayoongelewa sana kwa sasa ni hii picha na mtu anaefanana na Yesu




Amekua mtu wa kumiliki headlines kila anapokanyaga sasa hivi na tena uzito umeongezeka baada ya kuwekwa hadharani kwa uhusiano wake wa kimapenzi na TV Star Kim Kardashian.
Rapper Kanye West mwenye umri wa miaka 36 akiwa kwenye Tour yake ya ‘Yeezus’ alifanya watu wengi wazitumie sana camera zao kutokana na aina ya ubinifu uliotumiwa kwenye show yake huko Seattle Marekani.
Unaambiwa baadhi ya matukio ya show hii kwenye crowd ya zaidi ya watu elfu 17 ni wakati pia alipofanya show akiwa kwenye sehemu zilizotengenezwa kama milima lakini pia ambacho kilifanya camera za fans zitumike sana ni pale alipofanya show huku kwenye stage akiwa amepanda mtu anaefanana na Yesu, huyu ni mtu ambae tayari alikua ameandaliwa kwa ajili ya hii show ambayo set yake ilikua designed na kampuni ya Kenye, Donda Creative.


Kanye na mikono ya Mashabiki.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni